Search This Blog

Sunday, October 13, 2019

Kimbunga Hagibis chaitesa Japan

Juhudi za uokozi zimeshika kasi kuwafikia watu waliokwama kwenye maeneo yaliyokumbwa na mafuriko baada ya kimbunga kikali kuyapiga maeneo kadhaa ya Japan, ikiwemo mji mkuu, Tokyo.

Kimbunga Hagibis ambacho kimesababisha mvua kubwa na upepo mkali kiliwasili kusini mwa mji wa Tokyo jana Jumamosi kabla ya kuelekea upande wa kaskazini.

Kulingana na Shirika la Habari la Japan, kimbunga hicho tayari kimesababisha vifo vya watu 11 na zaidi ya majeruhi 100, huku watu wengine zaidi ya 17 bado hawajulikani waliko.

Picha za vidio zimeonesha helikopta ikiwaokoa watu katika eneo la Nagano ambalo limefurika maji baada ya kingo za mto Chikuma kupasuka.

Kiasi polisi na wanajeshi 17,000 wamewekwa tayari kwa ajili ya shughuli za uokozi huku mamlaka nchini Japan zikionya kuwa hatari ya kutokea maporomoko ya udongo bado ni kubwa.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...