Search This Blog
Sunday, October 6, 2019
Jela Miaka 3, Adai Alifanya Kosa Sababu ya njaa
Mahakama ya Wilaya ya Lindi, mkoani Mtwara, imemuhukumu mkazi wa Mitema aliyefahamika kwa jina la Kijazi Ally (29), kifungo cha miezi 36 jela baada ya kupatikana na hatia ya makosa mawili, likiwemo la kuvunja nyumba usiku na kuiba.
Kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo, mshtakiwa aliulizwa kama anazo sababu za msingi, zitakazoishawishi Mahakama isimpe adhabu kali kwa makosa aliyokutwa nayo, ambapo katika kujitetea kwake alikiri kosa hilo na kudai kuwa ilikuwa ni mara yake ya kwanza na alilitenda kwa sababu ya njaa na kuahidi kutorudia tena.
Baada ya utetezi huo, Hakimu Kiswaga alimuuliza Mwanasheria wa Serikali Godfrey Mramba, kama ana kumbukumbu ya makosa ya zamani kwa mshtakiwa,ambapo alijibu kuwa hana lakini aliomba apewe adhabu kali, kwani ni mwizi mzoefu anayesumbua wakazi wa Mji wa Lindi.
Mramba alisema licha ya kutokuwa na kumbukumbu kwa makosa ya zamani kwa mshtakiwa,lakini tayari anakabiliwa na kesi nyingine inayohusu vitendo vya uvunjaji wa nyumba za watu nyakati za usiku na ipo katika Mahakama hiyo.
Kufuatia kesi hiyo namba 14/2019, Hakimu Kiswaga alimhukumu mshtakiwa huyo kifungo cha miezi 36
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment