Search This Blog

Monday, October 28, 2019

CCM yawaonya wanaotumia rushwa kusaka uongozi


Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi ( CCM) Tanzania Bara, Philip Mangula amesema kuwa, chama hicho hakitamvumilia Mwanachama yeyote anayetumia rushwa kutafuta uongozi.

Mangula ametoa kauli hiyo mkoani Simiyu wakati wa kikao cha utoaji wa taarifa ya utekelezaji wa ilani ya CCM mkoani humo.

 "Hatutaki viongozi wapenda rushwa, tunataka watu wenye moyo wa kuwatumikia Wananchi, maana rushwa ni adui wa haki, yeyote atakayetumia fedha zake kununua kura hata kama atapata kura nyingi kiasi gani tutamfyekelea mbali," amesisitiza Mangula.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...