Search This Blog
Thursday, September 26, 2019
Yanga Yaandaliwa Mapokezi Mazito Zambia
KIKOSI cha Yanga kimeondoka Jana Jumanne kuelekea nchini Zambia tayari kwa ajili ya mchezo wa marudiano dhidi ya Zesco United ambapo Watanzania waishio nchini humo wamejipanga kuhakikisha wanaipa sapoti timu hiyo.
Yanga itarudiana na Zesco United siku ya Jumamosi mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika, katika mechi ya kwanza iliyopigwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar, timu hizo zilitoka sare ya bao 1-1.
Yanga inahitaji ushindi wa aina yoyote ili iweze kufanikiwa kusonga mbele katika hatua ya makundi ya michuano hiyo.
Akizungumza na Championi Jumatano, Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano wa Yanga, Rogers Gumbo alisema kuwa, kamati yake imejiandaa vyema kuhakikisha wanashinda mchezo huo ambapo kikosi kitaweka kambi ya siku moja Lusaka kisha kitaendelea na safari na kudai kuwa Watanzania waishio huko wameonyesha kuhamasika kwa kuipa sapoti timu yao.
“Hamasa ipo kubwa timu inaondoka kesho (jana) kuelekea Zambia na itafi kia Lusaka, itakaa siku moja kisha Alhamisi kikosi kitaondoka kuelekea Ndola tayari kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wetu.
“Kamati yetu imekutana na wachezaji katika kuwapa hamasa kuhakikisha wanafanikiwa kushinda mchezo huo ili kuingia hatua ya makundi ambayo ndiyo tageti yetu.
“Watanzania waishio Zambia wameonyesha ushirikiano wa hali ya juu kuelekea mchezo huo kutokana na sapoti yao, hivyo tuna imani tutapata matokeo mazuri,” alisema Gumbo
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment