Search This Blog
Monday, September 9, 2019
Wasanii wahakikishiwa kuondolewa vikwazo kurekodi kazi zao maeneo ya Hifadhi
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Kanyasu Constatine amewahakikishia wasanii wote nchini kuwa katika kipindi chake cha Uongozi ataondoa vikwazo vyote vilivyokuwa vinapelekea wasitumie madhari ya vivutio vya utalii vilivyopo nchini wakati wa kutengeneza kazi zao Sanaa.
Pia, Amewataka wasanii na watu maarufu wapende vitu vya kwao badala ya kuona ufahali wa kuitumia madhari za nchi nje ilhali Tanzania imejali kuwa kuwa utajiri wa mandhari za kipekee na zenye mvuto wa hali ya juu.
Akizungumza Jijini Dar es Salaam kwenye hafla iliyoandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kushirikiana na na vijana wa Tanzania Vision 2025 kwa kuwaalika watu maarufu hususan Wasanii kwenye chakula cha jioni, Naibu Waziri Kanyasu amewataka wasanii hao watumie kalama na ushawishi walio nao katika kuhamasisha utalii wa ndani.
Amewataka wasanii hao wasijione kuwa wao ni watu Wanyonge badala yake wajiamini kwa vile ni watu wenye ushawishi mkubwa katika jamii kupitia kazi zao za Sanaa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...


No comments:
Post a Comment