Search This Blog
Saturday, September 14, 2019
Waasi wa Houthi Wakiri Kuhusika na Shambulio la Vituo vya Mafuta Saudi Arabia
Ndege zisizokuwa na rubani ambazo waasi wa Houthi wamekiri kuzimiliki zimeshambulia eneo kubwa la kutengenezea mafuta nchini Saudi Arabia pamoja na eneo kubwa la mafuta linalomilikiwa na kampuni ya mafuta ya Aramco nchini humo na kusababisha moto mkubwa katika eneo muhimu la kusafirisha mafuta duniani.
Mpaka sasa haijawa wazi iwapo kuna majeruhi wowote katika shambulio hilo kwenye vituo vya mafuta vya Buqyaq na Khurais, au kujua ni athari za aina gani zitatokea katika shughuli za kuchimba mafuta nchini Saudi Arabia.
Shambulio hilo linaonekana kuongeza mvutano katika Ghuba ya Uajemi kutokana na mkwaruzano uliopo kati ya Marekani na Iran juu ya makubaliano yake ya nyuklia na mataifa yaliyo na nguvu duniani.
Waasi wa Houthi wanaungwa mkono na Iran katika mapambano ya zaidi ya mwaka mmoja dhidi ya kundi hilo mjini Yemen yanayofanywa na muungano wa kijeshi unaoongozwa na Saudi Arabia.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment