Search This Blog

Sunday, September 29, 2019

Unamkumbuka Mwigiza Nora ? Adai Amesahau Kama Alikuwa Staaa....


KUMBE kuna wakati unafika binadamu anasahau alikotoka? Msikie mwigizaji wa kitambo Bongo, Nuru Nassoro ‘Nora’, eti amesahau kabisa kama alishawahi kuwa staa wa sinema Bongo.

Nora ameliambia Gazeti la Ijumaa Wikienda kuwa, kwa sasa amebadilika kiakili hivyo hakumbuki kama alishawahi kuwa msanii kwani ni ishu ambayo hataki kabisa kuisikia kwa kuwa hivi sasa ameamua kumrudia Mungu mazima.

“Kuna vingine mtu hutamani hata kuvisikia maana vingi vilikuwa dhambi. Kichwani kwangu imeshafutika kabisa kama niliwahi kuwa staa wa sinema,” alisema Nora ambaye kwa sasa anafundisha maadili ya Dini ya Kiislam kama ilivyo kwa Mzee Yusuf aliyekuwa staa wa muziki wa Taarab nchini

STORI: IMELDA MTEMA,DAR

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...