Search This Blog
Thursday, September 5, 2019
Uhuru Seleman ajiunga na FC Lupopo
Mchezaji wa kitanzania Uhuru Seleman ameamua kuondoka klabu ya Royal Eagles ya Daraja la kwanza ya Afrika Kusini na kujiunga na FC Lupopo ya Ligi Kuu ya Congo kwa kandarasi ya miaka miwili.
Uhuru amesema kuwa amefikia maamuzi hayo kufuatia kuchoka kukaa mbali na familia yake na pia kuchoshwa na ubaguzi wa wageni (Xenophobia) unaoendelea nchini Afrika Kusini.
Kufuatia machafuko na ubaguzi huo, mchezaji huyo wa zamani wa Simba ameshindwa kuishi pamoja na familia yake nchi Afrika kusini, hivyo sasa amefikia maamuzi ya kuondoka.
“Sababu kubwa ya kuondoka ni kutokana na ubaguzi na machafuko ambayo hayaishi, kila siku tunapata vitisho, haviishi.” amesema Uhuru.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment