Search This Blog

Thursday, September 5, 2019

Uhuru Seleman ajiunga na FC Lupopo


Mchezaji wa kitanzania Uhuru Seleman ameamua kuondoka klabu ya Royal Eagles ya Daraja la kwanza ya Afrika Kusini na kujiunga na FC Lupopo ya Ligi Kuu ya Congo kwa kandarasi ya miaka miwili.

Uhuru amesema kuwa amefikia maamuzi hayo kufuatia kuchoka kukaa mbali na familia yake na pia kuchoshwa na ubaguzi wa wageni (Xenophobia) unaoendelea nchini Afrika Kusini.

Kufuatia machafuko na ubaguzi huo, mchezaji huyo wa zamani wa Simba ameshindwa kuishi pamoja na familia yake nchi Afrika kusini, hivyo sasa amefikia maamuzi ya kuondoka.

“Sababu kubwa ya kuondoka ni kutokana na ubaguzi na machafuko ambayo hayaishi, kila siku tunapata vitisho, haviishi.” amesema Uhuru.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...