Raisi wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa hatahudhuria mkutano mkuu wa umoja wa mataifa jijini New York, baadae mwezi huu.
Badala yake, amesema atabaki nchini humo kushughulikia changamoto zinazokabili nchi yake kwa sasa ikiwemo vitendo vya mashambulizi ya chuki dhidi ya raia wa kigeni na unyanyasaji dhidi ya wanawake
Nchini Afrika Kusini, miongoni mwa vichwa vya habari juma lililopita ilikuwa ni taarifa kuhusu ubakaji na mauaji ya wanawake na watoto katika sehemu kadhaa za nchi.
Iliwaacha wanawake wengi wakijiuliza: "Je! nitafuata mimi!
Kesi moja iliyemhusisha mtu mwenye hadhi kubwa, mfanyakazi wa ofisi ya posta ambaye alikiri kubaka na kumuua mwanafunzi wa miaka 19 Uyinene Mrwetyana. Ilikuwa ni wakati ambao uliwafanya wanawake kuhisi hatari na hofu.
Takwimu za hivi karibuni za uhalifu, ambazo zilitolewa Alhamisi, zilidhihirisha kwamba hofu yao ni dhahiri. Mauaji, ubakaji na unyanyasaji wa kijinsia vimeongezeka.
Lakini wanawake wengi wanakataa kunyamazishwa. Siku ya Ijumaa, mamia ya wanawake, ambao walikuwa wamevaa mavazi ya rangi nyeusi, walianza kukusanyika Johannesburg saa za asubuhi ili kuongeza uelewa dhidi ya dhuluma ya kijinsia.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment