Search This Blog

Thursday, September 5, 2019

Mwanamke akamatwa uwanja wa ndege akiwa amemficha mtoto wa siku sita kwenye begi


Maafisa wa uhamiaji wa Ufilipino wamemkamata mwanamke mmoja raia wa Marekani ambaye alikamatwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Ninoy Aquino akijaribu kumtorosha mtoto mchanga mwenye umri wa siku 6 akiwa amemficha kwenye begi lake.

Naibu msemaji wa idara ya uhamiaji ya Ufilipino, Melvin Mabulac alisema kuwa mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 43 alikuwa apande ndege ya kuelekea New York alipokamatwa baada ya mzigo wake kukaguliwa na mtoto huyo kugunduliwa.

 “Yule mtoto alikuwa amefichwa kwenye begi kubwa,” alisema Naibu msemaji wa idara ya uhamiaji ya Ufilipino.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...