Search This Blog
Monday, September 9, 2019
Mtoto wa miezi 5 akatwa kiganja, madaktari wadai damu ilivilia kumbe sumu
Mtoto wa miezi mitano Jijini Dar es salaam, katika hospitali ya Muhimbili amekatwa kiganja cha mkono wake wa kushoto baada ya kupatiwa huduma za matibabu ya sindano kupitia mshipa wa mkononi na kupelekea mkono huo kuharibika na kukatwa kabisa.
Matibabu hayo alikuwa akifanyiwa katika hospitali ya Mwananyamala ambapo baadae alipewa rufaa katika hospitali ya Muhimbili baada ya kuona hali ya mtoto inazidi kuwa mbaya na mkono ukizidi kubadilika rangi na kuwa mweusi huku ukisinyaa.
Mama wa mtoto huyo alianza kuona mkono wa mtoto wake ukibadilika lakini mara baada ya kuripoti hali hiyo kwa madaktari hospitali ya Mwananyamala walisema kuwa damu imevilia hivyo walimshauri mama huyu kuchukua mkono wa mwanae na kuweka kwapani hadi utaporudi katika hali ya kawaida.
Mama huyo alieleza hayo pindi alipohojiwa na chombo cha habari cha TBC, na kusema kuwa chanzo kilichopelekea mtoto wake kufikia hatua hiyo ni kutokana na kanyula aliyowekewa siku chache zilizopita alipofika kufanyiwa matibabu baada ya kushikwa na homa kali.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayeshughulikia Sekta ya Ujenzi, Arch. Elius Mwakalinga, akitoa maelekezo kwa Kai...

No comments:
Post a Comment