Search This Blog

Sunday, September 29, 2019

Mtalii afariki akiruka kwa Parachuti Mlima Kilimanjaro



Mtalii raia wa Canada, Justin Kyllo (51) amefariki baada ya Parachuti alilokuwa akitumia kuruka angani  kutoka kilele cha mlima Kilimanjaro nchini Tanzania kugoma kufunguka.

Kamishna msaidizi mwandamizi wa Hifadhi za Taifa (TANAPA), Pascal Shelutete amethibitisha kifo cha mtalii huyo, kwamba kimetokea katika kituo cha Stella Point kilichopo katika mlima huo.

Amesema mtalii huyo alifika Septemba 20 mwaka huu kwa ajili ya kupanda mlima, leo asubuhi alitumia Parachuti kwa ajili ya kuruka angani ili kushuka chini ya mlima lakini iligoma kufunguka na kusababisha kifo chake.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...