Search This Blog
Monday, September 23, 2019
Iran yaitaka Uingereza kuacha kuiuzia silaha Saudia
Iran imesema Uingereza inapaswa kuacha kuiuzia silaha Saudi Arabia, badala ya kuishutumu Jamhuri hiyo ya Kiislamu.
Kauli hiyo imetolewa leo baada ya Waziri Mkuu wa Uingereza, Boris Johnson kusema kuwa nchi yake inaamini Iran imehusika na mashambulizi katika vituo vya mafuta vya Saudi Arabia.
Msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa Iran, Abbas Mousavi amesema serikali ya Uingereza badala ya kuelekeza juhudi zisizozaa matunda dhidi ya Iran, inapaswa kuchukua hatua na kuacha kuuza silaha za maangamizi kwa Saudi Arabia, ambalo ni ombi la watu wengi duniani.
Kwa mujibu wa shirika la habari la Iran, Mousavi ameitaka Uingereza kujiondoa katika madai ya uhalifu wa kivita dhidi ya watu wa Yemen.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment