Halmashauri ya wilaya ya Bukoba Mkoani Kagera imefikisha zaidi ya 97% za ukusanyaji wa mapato kwa mwaka mzima ambayo ni zaidi ya shillingi bilion moja na zaidi ya milioni mia tatu.
Hayo yamesemwa na Mwenyeki wa halmashahuri ya Wilaya ya Bukoba Mh Murshid Ngeze katika kikao cha halmashahuri hiyo chenye lengo la kufunga robo ya nne ya mwaka wa fedha 2018/2019.
Mh Ngeze amesema kuwa halmashahuri hiyo imepiga hatua kubwa na kusema kuwa wakati wanaingia madarakani walikuwa wakikusanya zaidi ya shilingi milioni mia sita kwa mwaka lakini mpaka sasa wamevuka malengo kwa 100% kwa miaka minne wakiwa kwenye uongozi.
Ameongeza kuwa mafanikio hayo yamekuja kutokana na kasi ya Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dk John Pombe Magufuri ya usimamiaji mzuri wa rasirimali mbalimbali za nchi kitu kilichopelekea kila kiongozi kuwajibika kadri ya nafasi yake kuanzia ngazi ya juu mpaka ya chini kwa ajili ya maendeleo ya watanzania wote kwea ujumla.
Sanjali na hayo Mh Ngeze ambaye pia ni diwani wa kata ya Rukoma ameongeza kuwa wanafunzi wa kata hiyo wanaangaika kufata huduma ya elimu ambapo wanatembea takribani kilometa 38 jambo ambalo limepelekea kuanza ujenzi wa shule ya sekondari ili kuweza kutatua changamoto hiyo.

No comments:
Post a Comment