Search This Blog

Thursday, September 5, 2019

Ester: Wema Ameniumiza sana! Hadi nimekosa Raha Siku Nzima

Muigizaji wa Bongo Muvi, Ester Kiama amesema muigizaji mwenzake, Wema Isaac Sepetu amemuumiza roho hadi kumfanya aangue kilio na kukosa raha siku nzima. Ester ameyasema hayo kufuatia hivi karibuni Wema kumjibu mmoja wa mashabiki wake kwenye Mtandao wa Instagram ambaye alimsifia na kumuambia amekosa kitu kimoja tu bila kukitaja ndipo Wema alipomjibu; “ugumba.”


“Kwa kweli ile siku Wema aliniumiza sana. Hakuna siku ambayo nimejisikia vibaya kama siku ile nilivyoona hilo jibu la Wema kuhusu suala la ugumba, niliumia mno na siku yangu ikaharibika, yaani alinifanya siku yangu yoyote isipite bila kumuombea,” alisema Ester.

Kwa muda mrefu Wema amekuwa kwenye changamoto ya kutopata ujauzito, lakini hata hivyo hivi karibuni alikaririwa akisema tatizo hilo limeshatatuliwa na sasa anaweza kupata ujauzito.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...