Mtu mmoja anayedhaniwa kuwa ni jambazi ameuawa akijaribu kumpora paroko wa Kanisa Katoliki, Parokia ya Mtakatifu Theresa iliyoko Mbezi jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Ulinzi ya Jatu, Jacobo Mgwabati amewaeleza waandishi wa habari tukio hilo lilivyotokea, Jana, Septemba 6, 2019.
Ameeleza kuwa katika tukio hilo la uporaji, watuhumiwa walikuwa wawili na wote walikuwa na bastola. Alisema walimfuatilia Paroko akitokea benki na alipofika eneo hilo walimbananisha wakimlazimisha awape begi ambalo hata hivyo halikuwa na fedha.
Alisema kuwa watu hao walikuwa na pikipiki na walimuweka katikati Paroko huyo wakitishia kumuua.
“Paroko akaamua kuwapa begi baada ya kumtishia kumpiga risasi. Askari wetu akatumia busara, akaacha paroko asogee mbali nao kwanza, walipoondoka akawafyatulia risasi, moja ikampata mmoja wao kwenye kiuno akaanguka. Hakukaa sana akapoteza maisha na mwingine akakimbia kwa miguu,” Mgwabati anakaririwa na Mwananchi.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Mussa Taibu amemsifu mlinzi wa kampuni ya Jatu kwa kazi aliyoifanya kupambana na waporaji.
Kamanda Taibu amesema kuwa uchunguzi wa tukio hilo unaendelea na wanamtafuta mtuhumiwa aliyekimbia.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment