Search This Blog

Monday, August 12, 2019

Wellu Sengo Amtema STEVE Nyerere 'Mimi na Steve Biashara Imekwisha'

KAMA ulikuwa na mawazo kwamba huenda mwigizaji mahiri Bongo, Wellu Sengo na Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ wanaweza kuendeleza mapenzi, sahau! Mrembo huyo amezidi kusisitiza kuwa biashara imeisha.


Akizungumza na Gazeti la Ijumaa Wikienda, Welu ambaye wiki chache zilizopita aliweka wazi kwenye mtandao wake wa Instagram kuwa yupo ‘singo’ alisema kuwa siyo kitu kibaya kuandika vile kwa sababu kila mtu ana mtazamo wake.


“Kiswahili mara nyingi huwa kigumu, lakini ukweli ni kwamba Nyerere ni baba mtoto wangu na hakuna kingine zaidi ya hicho, watu waelewe na ninamshukuru Mungu hakuna kinachonisumbua kwa sasa,” alisema Welu.

STORI: IMELDA MTEMA,DAR

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...