Search This Blog

Friday, August 2, 2019

Waziri Mwakyembe akutana na kufanya mazungumzo na mjumbe toka Ligi ya Hispania

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe (kulia) akifafanua jambo kwa mjumbe kutoka La Liga nchini Hispania, Alvaro Paya wakati Mjumbe huyo alipomtembelea Waziri Mwakyembe na kujadiliana mambo mbalimbali ya kushirikiana ili kuinua soka la Tanzania.
Mjumbe kutoka La Liga nchini Hispania, Alvaro Paya (kushoto) akimwelezea Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe mikakati ya Shirikisho la nchi yake katika kuisadia Tanzania kufanya vizuri katika mchezo wa soka.
Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi nchini, Boniface Wambura (kushoto) akifafanua kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe (hayupo pichani) mikakati mbalimbali waliyofikia na Mjumbe kutoka La Liga nchini Hispania, Alvaro Paya (hayupo pichani) wakati mjumbe huyo alipomtembelea Waziri Mwakyembe leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe (kulia)akiagana na Mjumbe kutoka La Liga nchini Hispania, Alvaro Paya (kushoto) mara baada ya kumaliza kujadiliana mambo mbalimbali ya kushirikiana ili kuinua soka laTanzania.Picha na WHUSM-Dar es Salaam.


No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...