Search This Blog
Sunday, August 11, 2019
Watanzania 9 wahukumiwa kwenda jela nchini Marekani
Jumla ya Watu 11 kutoka nchi za Tanzania, Pakistani na Iran wamehukumiwa kifungo kwa kushiriki kusafirisha Dawa za Kulevya aina ya heroin nchini Marekani.
Watanzania waliohukumiwa ni Ali Khatib Haji Hassan (49), Makame Haji Mwinyi (49), Ernest Michael Mbwile (35), Abdulahtif Juma Maalim (43), Ibrahim Omary Madega (52), Tiko Emanuel Adam (41), Iddy Saleme Mfullu (46), Mohammed Said Mohammed (48) na Daud Michael Vedasto (58)
Wengine ni Salim Omar Balouch (36) kutoka Iran na Abdul Basit Jahangir (40) kutoka Karachi, Pakistan ambapo wote walihukumiwa Agosti 07, 2019 baada ya Jaji kusikiliza shauri lao kwa siku mbili mfululizo
Aidha, Jahangir amehukumiwa kifungo cha miezi 151, Mfullu na Mohammed wamehukumiwa kifungo cha miezi 50 kila mmoja huku Hassan akihukumiwa miezi 99, Mwinyi miezi 62, Mbwile miezi 52, Maalim miezi 46, Madega miezi 87, Adam miezi 37 na Vedasto miezi 46
Aidha, Mahakama imemuhukumu Balouch kifungo cha miezi 135 huku ikisema kuwa raia ambao si wa Marekani wanatarajiwa kusafirishwa kurudishwa nchini kwao baada ya hukumu hiyo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment