Baraza la Taifa la Sanaa (Basata) limesema wimbo Tetema wa msanii Raymond Mwakyusa maarufu Rayvanny aliomshirikisha Diamond Platnumz hauna tatizo lolote licha ya kuzuiwa kupigwa katika maeneo ya wazi nchini Kenya.
Kauli hiyo imetolewa leo Jumanne Agosti 27, 2019 na katibu mtendaji wa baraza hilo, Godfrey Mngereza alipoulizwa na Mwananchi kuhusu kupigwa marufuku kwa wimbo huo Kenya.
Mngereza amesema hauna shida na hajui Kenya wametumia vigezo vipi kuuzuia.
“Tumekuwa tukifuatilia nyimbo za wasanii wa hapa nchini na kuwaita wanapokosea. Tunatoa onyo na hata kufungia nyimbo zao, lakini huu (Tetema) hauna shida ndio maana nasema sijui wametumia vigezo gani kuuzuia usichezwe mchana,” amesema Mngereza.
Wimbo huo pamoja na Wamlabez wa msanii Sailors wa nchini Kenya zimezuiwa kupigwa maeneo ya wazi na badala yake zinatakiwa kupigwa katika kumbi za starehe na baa
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment