Search This Blog

Wednesday, August 28, 2019

Uganda yazindua kampeni ya kuchangia damu kufuatia ongezeko la malaria


Wizara ya afya nchini Uganda imezindua kampeni ya miezi mitatu ya kuchangia damu kufuatia ongezeko la ukosefu wa damu lililosababishwa na ongezeko la ugonjwa wa malaria nchini humo.

Akiongea katika shughuli za uzinduzi, waziri wa nchi anayeshughulika na huduma za afya Bibi Joyce Moriku Kaducu amesema kampeni hiyo inalenga kuongeza vitengo vya damu hadi elfu 50.

Kiwango hicho cha damu kinatarajiwa kupatikana kabla ya mwezi Novemba kutoka vitengo elfu 25 vya damu vya sasa. Pia amehamasisha wananchi kuchangia damu ili kuokoa maisha.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...