Search This Blog
Monday, August 5, 2019
Spika Ndugai awataka Watanzania kupanga familia kulingana na uchumi
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai amewataka watanzania kuwa na utaratibu wa kupanga familia kulingana na uchumi walionao.
Ameyasemayo jijini Dar es Salaam, baada ya kufungua mkutano wa wabunge kutoka bara la Asia na Afrika unahusu masuala ya idadi ya watu na maendeleo.
Akizungumza katika mkutano huo, Ndugai amesema kuwa wao kama bunge kazi yao kubwa ni kuishauri serikali katika sera mbalimbali ambazo zitasaidia katika kuhakikisha kunakuwa na idadi endelevu ya watu ambao wanaishi maisha marefu na pia yenye uchumi mzuri.
“Kuna baadhi ya nchi zilizoendelea sana kama Japani na kwingine ambako idadi ya watu sehemu kubwa ni wazee inategemewa idadi yao kupungua”.
“Uwe na idadi ya watu kuendana na uchumi wetu katika kiwango cha familia, kaya na baadae katika taifa kwa ujumla,”amesema Ndugai.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment