Search This Blog
Sunday, August 25, 2019
Serikali kufanya mageuzi makubwa kusimamia sekta ya sanaa na ubunifu
Katika kuboresha na kuleta mageuzi makubwa katika sekta ya Sanaa na Ubunifu (Art and Creative Industry) na kusogeza huduma kwa Wasanii na Wabunifu serikali ya awamu ya tano iko katika mchakato wa kuziunganisha taasisi zinazoshughulika na sekta hii na kuunda mamlaka moja.
Taasisi hizo ni Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Bodi ya Filamu na Chama cha hakimiliki na Hakishiriki (Cosota).
Kwa msingi huu Wasanii wa aina zote wakiwemo watunzi na waandishi mbalimbali, wabunifu, Waandishi wa habari na wadau wote wa Sanaa mnakaribishwa katika mkutano na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison George Mwakyembe pamoja na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Innocent Bashungwa utakaofanyika Siku ya Jumatano, Tarehe 28/08/2019 katika Ukumbi wa Julius Nyerere International Convention Center (JNICC) jijini Dar es Salaam kuanzia saa 3:00 Asubuhi.
Mbali na kujadili kwa kina mchakato wa uundwaji wa mamlaka moja ya kusimamia sekta ya Sanaa na Ubunifu kutakuwa pia na mazungumzo ya gawio la mirabaha kwa kazi za Wasanii wa muziki.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment