Search This Blog
Thursday, August 1, 2019
Rais wa nchi hii Afrika kusherekea miaka 40 madarakani
Rais wa Equatorial Guinea, Teodoro Obiang Nguema anasherehekea miaka 40 madarakani wiki hii. Nguema, 77 anatajwa kumuandaa mtoto wake Teodorin 51 ambaye ni Makamu wake wa Rais wa sasa kuja kushika madaraka.
Teodoro Obiang aliingia madarakani August 3, 1979 baada ya yeye na viongozi wengine askari kumpindua aliyekua Rais wa wakati huo ambaye ni mjomba wake dikteta Fransisco Macias Nguema.
Equatorial Guinea, taifa lenye kutegemea uchumi wa mafuta ni moja kati ya mataifa yanayotajwa kukithiri kwa rushwa, Makamu wa Rais na Mtoto wa Rais aliteuliwa kushika wadhifa huo 2012 huku 2017 akihukumiwa na mahakama moja nchini Ufaransa kwa makosa ya kumiliki mali nyingi zilizopatikana kwa udanganyifu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment