Search This Blog

Friday, August 16, 2019

Majeruhi Wengine Wanne Ajali ya Moto Morogoro Wafariki Dunia na Kufanya Idadi Kufikia 93


Majeruhi wengine wanne katika ajali ya moto iliyotokea Morogoro, Agosti 10, 2019 wamefariki Dunia, katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, na kufanya idadi ya waliofariki mpaka sasa kwenye ajali hiyo kufikia 93.

Vifo hivyo vinafanya idadi ya wagonjwa waliobaki kuwa 21 kati ya 46 waliokuwa wamefikishwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Dar es Salaam kwa ajili ya matibabu.

Akizungumza baada ya kutembelea wagonjwa hao leo Ijumaa Agosti 16, 2019,  Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto,  Ummy Mwalimu amesema madaktari wanafanya kila jitihada kuokoa maisha ya wagonjwa waliobaki.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...