Search This Blog

Tuesday, August 27, 2019

Majeruhi kuwaweka nje ya uwanja Kylian Mbappe na Cavani


Mshambuliaji nyota wa Paris Saint Germain, Kylian Mbappe atakuwa nje ya uwanja kwa wiki nne na mwenzake Edinson Cavani kwa wiki tatu baada ya wawili hao kuumia uwanjani katika mechi ya ligi kuu ya Ufaransa (Ligue 1) dhidi ya Toulouse.

Mbappe aliyekuwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Ufaransa kilichotwaa ubingwa wa dunia, alitoka baada ya kuumia misuli ya mguu wa kushoto wakati akichanja mbuga kwenye mechi hiyo ambayo PSG iliibuka na ushindi wa goli 4-0 kwenye uwanja wa Parc des Princes.

Mbappe huenda akakosa mechi ya ligi ya mabingwa Ulaya iliyopangwa kupigwa Septemba 17 au 18. Pia atakosa mechi tatu za ligi pamoja na mechi za Ufaransa michuano ya awali ya mataifa ya Ulaya, Euro 2020 dhidi ya Albania na Andorra zitakazofanyika Ufaransa mwezi ujao.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...