Search This Blog
Thursday, August 29, 2019
Madaktari wa China watibu watu milioni 220 Afrika
Kwa miaka 56 sasa, China imekuwa ikituma madaktari wake kutoa huduma za matibabu katika bara la Afrika. Kwa ujumla, taifa hilo la Asia limetuma madaktari 21,000 barani Afrika na kuweza kutibu jumla ya watu milioni 220.
Lin Xiaojun anatoka kwa moja ya familia za Wachina ambazo zimekuwa barani Afrika kwa vizazi vitatu zikitoa msaada wa matibabu.
“Kufanya kazi hapa Zanzibar kama daktari ni kitu cha kawaida katika familia yetu,” Lin ambaye aliwasili Zanzibar mwezi Julai alisema.
Ameendelea kwa kusema “Mnamo mwaka wa 1997, mama mkwe wangu Zhou Xiaoyu alikuwa hapa Zanzibar kwa muda wa miaka miwili katika operesheni ya kutoa msaada wa matibabu, mjomba wake Zhou Zhiyao naye alikuja hapa mwaka wa 1964 na 1977 pamoja na madaktari wa kutoka China,” alisema Lin.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...


No comments:
Post a Comment