Search This Blog
Sunday, August 11, 2019
Lugola aonya kuhusu ajali ya Lori Morogoro, ‘Tukio hili sio la kwanza’
Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amesema kuwa Watanzania hawana budi kujifunza kupitia tukio la ajali ya lori iliyopelekea vifo vya Watanzania zaidi ya 66.
Lugola ameyasema hayo mkoani Morogoro, ambapo amesema pindi ajali za namna hiyo zinapotokea, wananchi hawana budi kuviachia vyombo vya ulinzi na maafa kushughulika na masuala hayo.
“Tukio hili sio la kwanza kutokea na kujifunza, ila niseme Watanzania hatuna budi kujifunza, matukio ya namna hii yanayopotokea tuviache vyombo vya usalama na majanga ya ajali viendelee kushughulika, sisi wengine tukae pembeni,”amesema Lugola.
Aidha, Lugola amewaomba Watanzania kuendelea kuwa na utamaduni wa kuiheshimu sheria ya mitandao, na wao kama Serikali licha ya kukemea wataendelea kufuatilia watu wanaoendelea kuzisambaza picha zizizofaa mtandaoni.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment