Search This Blog
Sunday, July 28, 2019
Ubutu wa Mastraika Waiangusha Stars Nyumbani...
UBUTU wa safu ya ushambuliaji ta timu ya taifa, Taifa Stars iliyokuwa chini ya nahodha, John Bocco, umeinyima timu hiyo kupata ushindi nyumbani, licha ya kutawala sehemu kubwa ya pambano lao la kwanza kuwania tiketi ya Fainali za (Chan) za 2020.
Kocha Etienne Ndayiragije aliwaanzisha Bocco, Ayoub Lyanga na Idd Seleman 'Nado' huku akiwaweka benchi Salim Aiyee, Ibrahim Ajibu na Kelvin John aliowaingia kipindi cha pili katika pambano hilo la raundi ya kwanza lililopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Stars ilitawala mpira kwa asilimia 60 za kipindi cha kwanza hasa eneo la kiungo lililokuwa chini ya Jonas Mkude, Abubakar Salum 'Sure Boy' na Hassan Dilunga waliokuwa wakigawa mipira kiufundi wakisaidiwa na krosi za mabeki wa pembeni, Paul Godfrey na Gadiel Michael, lakini washambuliaji walikosa utulivu na kujikuta wakimaliza dakika 90 bila kufunga na Harambee ambao walionekana kuyahitaji matokeo hayo mapema tu.
Matokeo ya jana yanaiweka Stars katika mazingira magumu ya kusonga mbele katika mchezo wa marudiano utakaochezwa Agosti 4 mjini Nairobi.
Stars itajutia nafasi ambazo ilipata kipindi cha kwanza na kushindwa kuzitumia huku katika kipindi hicho ikifika langoni mwa Kenya mara nne huku Kenya ikifika mara mbili
Harambee Stars ilisubiri hadi dakika ya 13 kufanya shambulizi la kwanza lakini mabeki wa Stars wakiongozwa na Kelvin Yondani na Erasto Nyoni walikuwa makini na kumfanya kipa Juma Kaseja kutosukwasukwa langoni.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment