Search This Blog

Sunday, July 28, 2019

Roger Milla kupewa tuzo na FIFA

Mchezaji wa zamani Cameroon Albert Roger Mooh Milla, Septemba 7 atapewa tuzo na Shirikisho la Soka Duniani (Fifa) kwa kufunga bao akiwa na miaka 42.

Mpaka sasa imeshapita miaka 20 tangu nyota huyo apachk bao hilo kwenye michuano ya Kombe la Dunia.

Bao hilo alifunga kwenye mchezo wa timu yake ya Taifa ya Cameroon dhidi ya Urusi mwaka 1994 na kwa sasa ana umri wa 67

Tuzo hiyo itakuwa ni ya mfungaji mwenye umri mkubwa zaidi katika Kombe la Dunia na itatolewa Septemba 7 nchini Sweden.

Kwenye mchezo huo ambao ulichezwa uwanja wa Stanford nchini Marekani, Cameroon ilipoteza kwa kufungwa mabao 6-1 na timu ya Urusi ambayo nayo ilikuwa imeshatolewa kwenye michuano hiyo mikubwa.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...