Search This Blog

Tuesday, July 23, 2019

GAVANA SHILATU ATEMBELEA MAGHALA YA UFUTA



Na Mwandishi wetu Mihambwe

Afisa Tarafa Mihambwe Ndugu Emmanuel Shilatu ametembelea Maghala ya vyama vya msingi yanayopokea ufuta kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani ya Mihambwe na Michenjele yaliyopo Tarafa ya Mihambwe ili kujionea utaratibu unaotumika.

*"Kazi ya Serikali ni kuwasimamia, kuona mambo yanaenda vyema. Nimekuja kuwatembelea ili kuona changamoto zilizopo ili kuzitatua na pia kujiridhisha na utaratibu unaotumika. Kwa taarifa mlizonipatia mnakiri malipo yanaenda vyema kwa ufuta uliouzwa tayari. Kwa upande wa Mnunuzi ajitahidi sana kuja kuuchukua mzigo wake kwa wakati mara tu afanyapo malipo."* alisisitiza Gavana Shilatu. 

Wakulima wanaendelea kujitokeza kwa wingi kuleta ufuta ghalani na hadi sasa minada minne mikubwa imefanyika ya kuuza ufuta ambapo 60% ya makusanyo yote mpaka sasa yameshauzwa na Wakulima wameshalipwa fedha zao.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...