Search This Blog

Wednesday, July 3, 2019

CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) CHAKABIDHI BAISKELI YA UMEME KWA KIJANA MWENYE ULEMAVU

Akiwa katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Lumumba Dar es salaam Ndg. Ngemela Lubinga Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Kwa niaba ya Ndg. Bashiru Ally Katibu Mkuu wa CCM, amekabidhi baiskeli ya umeme ( Electric Wheelchair ) kwa Kijana mwenye ulemavu ili kuhamasisha moyo wa kujitolea kwa wenye uhitaji.

Akifafanua uamuzi huo wa CCM Ndg. Lubinga amesema Chama kilipokea maombi ya mahitaji ya baiskeli ya watu wenye ulemavu kutoka kwa Ndg. Yusuph Samweli kijana mwenye ulemavu wa miguu ili apate wepesi wakushughulika na shughuli mbalimbali ikiwemo masomo yake ya Sekondari. 

"Baiskeli hii imetengenezwa na kiwanda chetu cha ndani, tuvitumie viwanda vyetu vya ndani, watanzania wanaweza na Tanzania ya Viwanda imewezekana" amesisitiza Ndg. Lubinga

Huu ni muendelezo wa utekelekezaji wa kazi za Chama ndani ya Jamii Nje ya chama.

Imetolewa na:
IDARA YA ITIKADI NA UENEZI
CHAMA CHA MAPINDUZI




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...