Search This Blog
Wednesday, July 10, 2019
Benki ya Dunia yazindua shindano la vijana kukabiliana na ukosefu wa ajira
Shindano la vijana kuhusu biashara linaloungwa mkono na Benki ya Dunia kwa lengo la kukabiliana na tatizo la ukosefu wa ajira limezinduliwa nchini Kenya.
Mkurugenzi wa Benki ya Dunia kwa nchi za Eritrea, Kenya, Rwanda na Uganda Bw. Carlos Felipe Jaramilo, amewaambia wanahabari mjini Nairobi kuwa benki hiyo imetenga dola milioni 13.5 kwa ajili ya shindano la mpango wa biashara la Mbelena, ambalo litatoa mtaji kwa watu 750.
Amesema shindano hilo litakalofanyika katika nchi nzima, litawalenga vijana wenye mawazo ya kufanya biashara, au ambao tayari wana biashara, na lengo lake ni kutengeneza nafasi za ajira kwa vijana.
Amesema shindano hilo litawalenga zaidi wanawake ambao huwa hawashiriki sana kwenye mashindano kama hayo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment