Search This Blog

Friday, July 19, 2019

AZAM FC WATINGA FAINALI YA KAGAME CUP

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Azam FC imefanikiwa kutinga fainali ya Kombe la Kagame kwa mara ya tatu mfululizo baada ya kuwaondosha kwa mikwaju ya penati As Maniema Union ya DR Congo.

Mchezo huo uliokuwa wa kasi na ushindani, ilichukua dakika 120 kuweza kupatikana kwa mshindi atakayeenda kucheza na KCCA ya Uganda kwenye mchezo wa fainali.

Azam ambao ndio mabingwa watetezi wakiwa wamelichukua mara mbili mfululizo watacheza fainali ya nne kihistoria siku ya Jumapili.

Katika Mikwaju ya Penati, Azam walifanikiwa kufunga penati 5-4 kufuatia dakika 120 kumalizika kwa suluhu. 

Mabingwa hao watetezi wa michuano hiyo mara mbili mfululizo, watacheza fainali hiyo dhidi ya KCCA ya Uganda Jumapili hii.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...