Search This Blog

Sunday, June 9, 2019

Undertaker amshushia kipigo kizito Goldberg


Usiku kuamkia Jumamosi ya wikiendi iliyomalizika, mwanamieleka William Calaway maarufu kama Undertaker amemcharaza mpinzani wake William Scott maarufu kama Goldberg katika mchezo wa Super Showdown nchini Saudi Arabia.

Awali kabla ya mchezo huo, tambo za wababe hao zilivuta hisia za mashabiki wengi kutokana na rekodi za wawili hao katika medani ya mchezo huo wa mieleka.

Mchezo huo ulidumu kwa dakika 24, Undertaker akipigwa mara tatu lakini haikufanya kumzuia Undertaker kuibuka mshindi wa pambano hilo.

Matokeo mengine, Randy Orton amemshinda Tripple H, Braun Strowman amemtandika Bobby Lashley huku bingwa wa WWE Kofi Kingston ametetea ubingwa wake dhidi ya Dolph Ziggler.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...