Search This Blog

Saturday, June 22, 2019

Misri Yafungua Dimba na Ushindi Mwembamba Yaifunga Zimbabwe Bao 1-0

Wenyeji wa michuano ya Afcon, Misri wameanza michuano hiyo kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Zimbabwe.

Mechi hiyo ya ufunguzi wa michuano ya Afcon kwenye Uwanja wa Taifa jijini Cairo, Misri walikwenda mapumziko wakiwa na bao 1-0, mfungaji akiwa Mohamed Trezeguet.

Hata hivyo, Khama Billiat wa Zimbabwe ndiye alikuwa msumbufu zaidi upande wa ngome ya Misri na wenyeji walilazimika kufanya kazi ya ziada kupata bao.


Zimbabwe walionekana kucheza kwa kujiamini lakini tatizo likawa ni mashambulizi dhaifu.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...