Search This Blog
Saturday, June 29, 2019
Maskini Watanzania TISA Wauawa na Wengine Kujeruhiwa Mpakani mwa Msumbiji..Kisa Hichi Hapa
Raia tisa wa Tanzania pamoja na raia wawili wa Msumbiji wameuawa na watu wasiojulikana huku Watanzania wengine sita wakijeruhiwa vibaya katika kijiji cha Mtole kilichopo upande wa Msumbiji mpakani mwa Tanzania na Msumbiji.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchni, IGP Saimoni Siro amefika mkoani Mtwara kufuatilia tukio hilo lililotokea Juni 26, 2019 na kusema msako unaanza mara moja kwa kushirikiana na Serikali ya Msumbiji ili kuwakamata watu waliohusika na mauaji hayo.
Wakizungumzia tukio hilo majeruhi waliolazwa katika hospitali ya rufaa ya Ligula wamesema kuwa watu hao waliofanya mauaji walikuwa saba na waliwalaghai wananchi kwa kuitisha mkutano na kuanza kuwashambulia.
Wajeruhi hao wameiomba Serikali kuhakikisha inawakamata wauaji hao. Mauaji hayo yalitokea wakati Watanzania hao kutoka Kijiji cha Kihamba upande wa Mtwara wakiwa kijijini hapo kwa shughuli za kilimo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment