Search This Blog

Sunday, June 23, 2019

Kamati ya amani na usalama ya Umoja wa Afrika kufanya mkutano leo


Waziri wa mambo ya nje wa Morocco juzi alitangaza kuwa, kamati ya amani na usalama ya Umoja wa Afrika itafanya mkutano leo mjini Skhirat.

Mkutano huo wa siku tatu utakagua hatua za ujenzi wa amani barani Afrika, njia ya kufanya kazi ya kamati hiyo na changamoto za kutatua mgogoro barani Afrika.

Mkutano huo utahudhuriwa na nchi wanachama 15 wa kamati hiyo, zikiwemo Algeria, Angola, Burundi, Djibouti, Gabon, Guinea Ikweta, Kenya, Lesotho, Liberia, Nigeria, Rwanda, Sierra Leone, Togo, Zimbabwe na Morocco.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...