Search This Blog
Thursday, May 23, 2019
WHO yazindua mpango wa dunia kukabilia na kung'atwa na nyoka
Shirika la afya duniani WHO, hii leo limezindua mkakati mpya unaolenga kupunguza vifo na majeraha yanayotokana na kung'atwa na nyoka, likionya kuwa ukosefu wa dawa za kuuwa sumu unaweza kusababisha dharura ya kiafya.
Kila mwaka, karibu watu milioni tatu hung'atwa na nyoka wenye sumu, na karibu watu kati ya elfu 81 na laki moja na 38 elfu hufariki dunia. Manusura wengine 400,000 hukumbwa na ulemavu wa kudumu na madhara mengine, kwa mujibu wa takwimu za WHO.
Katika ripoti yake mpya, shirika hilo la afya la dunia limeihimiza jumuiya ya kimataifa kuchukua hatua kushughulikia tatizo hilo, ambalo linasema limepuuzwa kwa muda mrefu.
http://bit.ly/2M4oQQE
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment