Search This Blog
Thursday, May 30, 2019
Utabiri wa hali ya hewa waonyesha dhoruba zaidi kutokea Marekani
Watabiri wa hali ya hewa Marekani wanaonya juu ya uwezekano wa kutokea dhoruba hatari zaidi kwenye maeneo ya katikati ya nchi, inayoambatana na upepo mkali katika maeneo ambayo yalishuhudia hali ya hewa mbaya sana Jumatatu usiku.
Idara ya hali ya hewa Marekani-NWS imeeleza Jumanne vimbunga takribani 53 ambavyo huenda vimepiga usiku kucha, vimeuwa mtu mmoja na kuwajeruhi wengine 90.
Ripoti za dhoruba zilibandikwa kwenye mtandao na kitengo cha utabiri wa majanga cha taifa, zimeeleza kwamba vimbunga vilivyotabiriwa 14 vilipiga kwenye jimbo la Indiana, 11 Colorado na tisa Ohio.
Vimbunga 6 viliripotiwa kwenye jimbo la Iowa, vitano Nebraska, vinne huko Illinois, vitatu Minnesota na kimoja kwenye jimbo la Idaho.
Dhoruba hiyo iliharibu nyumba, kung’oa miti na kuangusha nguzo za umeme na kupelekea vifusi vingi ambavyo timu ya wasafishaji iliwabidi kutumia vifaa vya kuzolea theluji kusafisha barabara kuu huko Ohio.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment