Search This Blog
Thursday, May 23, 2019
UNAJUA Kuwa Kitunguu Swaumu & Tangawizi ni Msaada kwa Wenye Pumu..!!!?
Pumu ni tatizo la kupumua ambalo mara nyingi huwapata watoto na hata watu wazima kutokana na hitilafu mbalimbali katika mfumo wa kupumua.
Pumu huweza kusababishwa na kuvimba kwa kingo za mirija ya kuvuta hewa, matatizo ya mzio (allergy), matatizo ya uyeyushaji wa chakula ndani ya tumbo pamoja na matatizo ya kisaikolojia.
Tatizo hili la pumu likishughulikiwa vizuri kwa watoto wadogo huweza kuisha kabisa.
Mara nyingi tiba ya pumu huwa hailengi katika kuponya kabisa bali husaidai kufifisha nguvu ya mashambulio ya pumu pale yanapotokea, pia kumbukuza kwa kiasi kikubwa idadi ya mashambulio ya pumu kwa mgonjwa.
Moja ya njia inayoweza kutoa ahueni kwa mgonjwa wa pumu ni pamoja na hii ya kutumia tangawizi na kitunguu swaumu.
Unachopaswa kufanya ni kukatakata na kuponda punje tatu za kitunguu swaumu zilizochanganywa na kiasi kilicholingana na cha tangawizi. Kisha chemsha katika maji glasi moja na unywe kila jioni kabla ya kulala. Fanya hivyo mara mbili kwa siku asubuhi na jioni
http://bit.ly/2W0peUP
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment