Search This Blog

Thursday, May 23, 2019

Singida United wapishana na mamilioni


Baada ya timu ya Singida United kufungwa mabao 2-0 na Simba juzi Uwanja wa Namfua uongozi wa Singida United umesema kuwa wamepishana na mamilioni ambayo yalitengwa kwa ajili ya ushindi wao.

Ofisa Habari wa Singida United, Cales Katemana ameeleza kuwa waliwaambia wachezaji wao kwamba endapo watashinda kila mmoja angepata kiasi cha shilingi laki mbili na viongozi wa mkoa waliongeza dau kufikia milioni kwa atakayefunga bao.

"Haikuwa bahati yetu na wachezaji wetu walipambana wameshindwa hivyo wamepishana na fedha ambazo zilikuwa zimetengwa kwa ajili yao kwani mbali na milioni sita ambazo zilitengwa na timu viongozi na wadau waliweka mezani milioni moja kwa kila bao.

"Kila kitu kilikuwa wazi maana mchezo wa mpira haufichiki, hivyo hamna namna nyingine wachezaji wamekosa milioni kwa kuwa hakuna aliyefunga, kasi yetu tunailekeza kwenye mchezo wetu wa mwisho dhidi ya Coastal Union utakaochezwa mkoani Tanga," amesema Katemana.

http://bit.ly/2X71xqA

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...