Search This Blog
Friday, May 24, 2019
Serikali yajiwekea mkakati wa kupanda miti Mi. 280 nchi nzima
Serikali imeweka mkakati wa kupanda miti Milioni 280 kati ya mwaka 2016/20 katika maeneo mbalimbali nchini.
Kauli hiyo aliitoa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Costantino Kanyasu wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Same, Magharibi, Nagenjwa Kaboyoka (Chadema).
Mbunge huyo alitaka kujua kama serikali inaweza kwenda kushauriana na wananchi wa vijiji jimboni kwake ili kutenga maeneo kwa ajili ya kuanzisha misitu ya vijiji.
Kanyasu alisema serikali haina kipingamizi kushirikiana na vijiji katika kutenga maeneo kwa ajili ya kuanzisha misitu ya kijiji lakini mara nyingi baadhi ya wananchi wamekuwa wakifanya hivyo na baadaye wanageuka na kudai maeneo yao.
Alisisitiza kuwa endapo wananchi wa jimbo na mbunge huyo wapo tayari, basi serikali itashirikiana nao. Akijibu swali la msingi la Kaboyoka aliyetaka kujua serikali ipo tayari kuanzisha mradi wa utunzaji mazingira katika kata za Bendera, Kihurio, Ndungu na Maore ili kuhifadhi mazingira. Kanyasu alisema wilaya ya Same kiikolojia na kijiografia imegawanyika katika kanda kuu mbili yaani ukanda wa milima ambao hali yake ya hewa ni nzuri ukilinganisha na ukanda wa tambarare ambapo hali ya hewa ni ukame.
http://bit.ly/2wiJIca
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...
No comments:
Post a Comment