Search This Blog
Thursday, May 30, 2019
RC Makonda kuwasaka wasiona vitambulisho vya ujasiliamali
Mkuu waMkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda ametangaza msako kwa wafanyabiashara wadogo wasiokuwa na vitambulisho vya ujasiliamali vilivyo anza kutolewa mapema mwanzoni mwa mwaka huu.
Msako huo ni moja ya mkakati wa ukusanyaji mapato kupitia wafanyabiashara hao.
Paul Makonda amesema Juni 3 mwaka huu ni marufuku kwa mfanyabiashara yoyote mdogo kujishughulisha na biashara ndani ya mkoa huo bila kuwa na kitambulisho maalumu cha utambuzi kilichotolewa na Rais Dk John Magufuli.
Sambamba na hilo,mkuu wa mkoa huyo amewasihi wafanyabiashara hao walipe kodi ili waongeze wastani wa pato la taifa kupitia kodi.
Aidha Makonda amewataka wafanyabiashara wasiopata vitambulisho lakini wanavigezo vya kuvipata wafike sehemu husika ikiwemo ofisi za wakuu wa mikoa ili kuvipata.
Amesema takwimu kubwa zinaonyesha kuwa idadi ya wafanyabiashara wasiokuwa na vitambulisho ni kubwa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...

No comments:
Post a Comment