Search This Blog
Monday, May 27, 2019
Rais Afrika Kusini ahitaji walimu Tanzania
Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa amemhakikishia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kuwa atachukua walimu wa Tanzania kwa ajili ya kufundisha Kiswahili nchini kwake.
Rais Magufuli amehakikishiwa hilo leo, Mei 26, alipotembelea Ikulu Jijini Pretoria kufanya mazungumzo na Rais Ramaphosa, ikiwa ni siku moja baada ya kuapishwa kuwa Rais wa Awamu ya Tano wa nchi ya Afrika Kusini.
Pamoja na mambo mengine, Rais Magufuli amempongeza Rais Ramaphosa kwa kuapishwa na kumhakikishia kuwa Tanzania itaendeleza uhusiano wa kidugu na kihistoria na nchi hiyo, ulioasisiwa na Baba wa Taifa, Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere na Hayati Nelson Mandela.
Katika salamu zake za kumshukuru Rais Magufuli kwa kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwake, Rais Ramaphosa amesema kufuatia uamuzi wa Afrika Kusini kuanza kufundisha Kiswahili, nchi yake itachukua walimu wa Kiswahili kutoka Tanzania ili wafundishe somo hilo katika shule za msingi na sekondari nchini humo.
http://bit.ly/2W3Ngyo
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment