Search This Blog
Wednesday, May 29, 2019
Namna Kagera Sugar na Stand United walivyoshuka daraja
Ni rasmi timu za African Lyon ya Dar es Salaam na Kagera Sugar ya Kagera zimeshuka daraja kutoka Ligi Kuu Soka Tanzania Bara na msimu ujao zitacheza Ligi Daraja la Kwanza.
Mwadui FC na Stand United za Shinyanga zitacheza mechi za mtoano dhidi ya timu za Geita Gold FC na Pamba SC kuamua kubaki au kuondoka kwenye ligi kuu.
African Lyon imemaliza ligi ikiwa mkiani na pointi 23 huku Kagera Sugar ikiwa na pointi 44, sawa na Stand United na Mwadui wakitofautiana kwa idadi ya magoli ya kufunga na kufungwa huku matokeo baina ya Kagera Sugar na Stand mara mbili walizokutana (Head-to-Head) pia yakichangia anguko hilo la Kagera Sugar
Mwadui itacheza mtoano na Geita Gold ya Daraja la Kwanza huku Stand ikitarajiwa kucheza na Pamba kuwania kubaki ligi kuu, wakati wapinzani wao wakiwaniA kupanda daraja.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment