Rais wa Malawi Peter Mutharika amethibitishwa na tume ya uchaguzi kunyakua muhula wa pili madarakani baada ya kupata ushindi mwembamba wa asilimia 38.7 ya kura.
Mwenyekiti wa chama cha upinzani cha Malawi Congress Party Lazarus Chakwera, ameibuka nafasi ya pili na asilimia 35.41 ya kura wakati makamu wa rais Saulos Chilima akipata asilimia 20.24.
Uchaguzi wa rais na wa bunge ulifanyika Jumanne iliyopita, ambapo matokeo yalitarajiwa kutolewa mwishoni mwa Juma.
Hata hivyo tume ya uchaguzi ya Malawi ilisitisha kutangaza matokeo ya mwisho siku ya Ijumaa baada ya mahakama kuu kuamuru hivyo kutokana na malalamiko 147 yaliyowasilishwa ya hitilafu katika uchaguzi ikiwemo karatasi za kupigia kura zilizokuwa zimefutwa kwa kutumia wino wa kufanya masahahisho.
Baadae Jumatatu mahakama iliondoa amri hiyo na tume ya uchaguzi kuthibitisha ushindi mwembamba wa Mutharika.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment