Search This Blog
Tuesday, May 28, 2019
Mbwana Samatta Aingia Kwenye 10 Bora Ulaya
NA ELBOGAST MYALUKO
Baada ya ligi 5 bora barani Ulaya kumalizika kwa msimu 2018/19, wafungaji wa magoli wameongozwa na Lionel Messi, ambaye amechukua kiatu cha dhahabu nchini Hispania pamoja na Ulaya baada ya kufunga magoli 36 kwenye La Liga.
Wakati Messi akifunga mabao 36 ni mchezaji mwingine mmoja tu ambaye amefunga magoli zaidi ya 30, ambaye ni Kylian Mbappé wa Paris Saint-Germain, aliyefunga 33, huku washambuliaji wengine wakifunga kuanzia magoli 20 akiwemo Mbwana Samatta.
Wachezaji waliofikisha magoli 20 msimu huu kwenye ligi tano bora Ulaya.
LA LIGA
Messi 36
Benzema na Suarez 21
EPL
Mohamed Salah 22
Aubameyang 22
Sadio Mane 22
LIGUE 1
Kylian Mbappé 33
Nicolas Pépé 22
BUNDESLIGA
Robert Lewandowski 22
SERIE A
Fabio Quagliarella 26
Duván Zapata 23
Krzysztof Piatek 22
Cristiano Ronaldo 21
Kwa upande wa Ligi kuu ya Ubelgiji nahodha wa taifa Stars Mbwana Samatta, amefunga jumla ya magoli 23 hivyo kuwa amezidiwa na wachezaji watatu tu ambao ni Messi, Mbappe na Quagliarella huku akilingana na Duván Zapata.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment