Search This Blog

Thursday, May 30, 2019

Mbunge ataka REA iunde tume maalum kusimamia miradi ya umeme


Mbunge wa Viti Maalumu, Upendo Peneza (CHADEMA), ameitaka Wizara ya Nishati kuunda kitengo maalumu cha kusimamia miradi ya umeme ya Wakala wa Umeme Vijijini (REA).

Kauli hiyo ameitoa leo, bungeni jijini Dodoma, wakati akichangia mjadala wa Wizara ya Nishati kwa mwaka 2019/20 ambapo amesema kumekuwa na changamoto katika usimamizi wa miradi ya Rea.

“Mradi wa Rea mnachelewesha  fedha hatimaye inazalisha ongezeko la fedha kwa wasimamizi wa miradi, hata wale wanaofanya hizo kazi wapo wanaochelewesha.

“Naiomba Wizara iunde kitengo maalumu kwa ajili ya kushughulikia miradi yote ya Rea kuepusha changamoto hizo,” amesema.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...