Search This Blog

Tuesday, May 28, 2019

Lazaro Nyalandu akamatwa na TAKUKURU


Baada ya kuenea kwa Taarifa nyingi katika Mitandao ya kijamii kukamatwa kwa Waziri wa Maliasili na Utalii Mstaafu, Lazaro Nyalandu. Hatimae Kamanda wa Polisi amethibitishaa.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida amesema Lazaro Nyalandu anashikiliwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoani Singida na sio Jeshi la Polisi.

Kwa upande wake,Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje (CHADEMA), John Mrema kupitia ukurasa wake wa Twitter ameandika "TAKUKURU wamempeleka Polisi Lazaro Nyalandu na wenzake baada ya kumkuta hana makosa ya rushwa. Hatujui huko Polisi amepelekwa ili akatafitiwe makosa gani mapya. Hivyo yuko kituo cha Polisi Kati Singida."

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...